.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 8 Januari 2015

WANANCHI WA MVOMERO WAMTAKA MBUNGE WAO MH AMOS MAKALLA AGOMBEE TENA UBUNGE JIMBONI HUMO


Mbunge wa jimbo la Mvomero mkoani Morogoro, Mh Amos Makala mwenye shati maua akicheza ngoma wakati akipokelewa kijiji cha Manza wilayani Mvomero. 

Mh Makalla amepokelewa kwa shangwe na wananchi wa jimbo lake ambapo wamemtaka agombee tena ubunge katika uchaguzi ujao. Wananchi hao hawakusita kusifia utendaji wake mzuri, mchapakazi, mkweli na amefika vijiji vyote 130 jimboni kusikiliza na kutatua kero za wananchi. 

Katika ziara hiyo, Mh Makalla alishiriki chakula na walemavu katika kijiji cha Chohero na kuwakabidhi mbuzi kumi wa maziwa na nyama, pia alizindua na kukichangia kikundi cha kikoba cha faidika kijiji cha Manza, alisimamia uchimbaji wa kisima kijiji cha Kimambila-Mzumbe.
Mbunge wa jimbo la Mvomero mkoani Morogoro, Mh Amos Makalla akikabidhi kikundi cha Faidika kijiji cha Manza mchango wa shilingi laki tano tasilimu.
Mh Makalla akiwa amesimama kuwasalimia na kuzungumza na vijana katika kijiji cha Manza, Mvomero.
Mbunge wa jimbo la Mvomero ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maji, Mh Amos Makalla akikabidhi mbuzi kumi kwa ajili ya walemavu kumi waa kijiji cha Chohero- Mvomero.
Mbunge wa Mvomero ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maji, Mh Amos Makalla akihutubia mkutano katika kijiji cha Kimambila.
Umati wa wananchi ukimsindikiza Mbunge wao, Mh Amos Makalla akiwemo mtoto aliyemshika mkono ambao walifurahia kuona gari likichimba kisima kirefu cha maji katika kijiji cha Kimambila.
Mh Makalla akifurahia jambo na wapiga kura wa jimbo lake alipokuwa katika ziara jimboni mwake.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni