.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 16 Februari 2015

AFYA YA BOBBY KRISTINA BADO SI NZURI LICHA YA USIRI KUTAWALA

Afya ya mtoto wa staa wa muziki Bobby Brown, Bobbi Kristina imeripotiwa kutokuwa na mabadiliko yoyote, taarifa inayokingana na ripoti zinazoendelea kusambaa kuwa baadhi ya viungo vyake vimeanza kuacha kufanya kazi na kuhatarisha zaidi uwezekano wa yeye kuendelea kuishi.

Chanzo cha karibu kabisa kutoka familia ya binti huyo kimeeleza kuwa, kumekuwa na changamoto kubwa ya kuibuka kwa habari za kupotosha kuhusu afya ya Bobbi Kristina, hali yake ikiwa haina mabadiliko yoyote huku familia ikiendelea kuwa karibu naye na matumaini ya kuimarika kwa afya yake yakiwa pale pale.

Bobbi Kristina ameendelea kupumua kwa msaada wa mashine tangu alipopatikana akiwa hajitambui katika sinki ya bafu nyumbani kwake Januari 31 mwaka huu.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni