.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 16 Februari 2015

MISRI YAJIBU MAPIGO KWA MASHAMBULIZI BAADA YA RAIA WAKE 21 KUUWAWA NA IS

Misri imesema imeshambulia maeneo ya kundi la Dola ya Kiislam (IS) nchini Libya, ikiwa ni saa chache tu kupita baada ya kutokea tukio la kukatwa vichwa raia wake 21 Wakristo.

Televisheni ya taifa ya Misri, imesema mashambulizi hayo yamelenga kambi, maeneo ya mafunzo na maeneo ya kuhifadhi silaha ya kundi hilo.

Mapema rais Abdel Fattah al-Sisi amesema Misri inahaki ya kujibu mapigo dhidi ya mauaji ya raia wake yaliyofanywa na kundi la IS nchini Libya.
             Ndugu wa raia wa Misri waliouwawa wakiandamana kuonyesha hasira zao

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni