Naibu Waziri wa Maji,Mh Amos Makalla ameendelea na ziara yake na leo
ametembelea wilaya ya Siha kwa kuongea na viongozi wa wilaya ya Siha,
kutembelea miradi ya maji kijiji cha Emburukoi, Kijiji cha Kandashi na
bodi za maji za Lawale Fuka na Magadini Makiwarau.
Amezipongeza bodi za maji za Lawate Fuka na Magadini Makiwarau kwa
kujiendesha vizuri na kutoa huduma kwa ubora wa hali ya juu kwa wananchi
zaidi ya 100,000
Aidha amezitaka bodi za maji za daraja C na kamati za maji kufika wilaya ya Siha kujifunza
Kuhusu mradi wa kutoa maji mto simba kupeleka Longido ameagiza viongozi
wa wilaya ya Siha na Longido, watalaamu wa bonde la kati na Pangani na
ofisi ya katibu Tawala mkoa wa Arusha kuwa na vikao vya ujirani mwema
wakati huu ambao wizara ya maji inatafuta fedha za kutekeleza mradi huo.
Naibu Waziri wa Maji, Mh Amos Makalla akisalimiana na viongozi wa chama cha mapinduzi wilaya ya Siha.
Naibu Waziri wa Maji, Mh Amos Makalla akiangalia kituo cha kuchotea maji Sanya Juu.Naibu Waziri wa Maji, Mh Amos Makalla akikagua ujenzi wa tanki kijiji cha Embukoi.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni