Ndege ndogo ya mazoezi ya jeshi la
wananchi Tanzania (JWTZ) imeanguka asubuhi ya leo katika uwanja wa
ndege wa Mwanza, wakati ikijaribu kuruka.
Kwa mujibu wa mwandishi wetu rubani
wa ndege hiyo ambaye jina lake halijapatikamara moja alinusurika
baada ya kuvunja kioo na kuruka nje ya ndege hiyo.
Inadaiwa chanzo cha ajali hiyo ni
ndege aliyekuwa ameingia kwenye mfumo wa injini ya ndege hiyo, hata
hivyo maafisa wa JWTZ waliokuwepo eneo la ajali hawakutaka
kuzungumzia ajali hiyo.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni