.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 19 Februari 2015

RAPA VANILLA ICE AKAMATWA NA KUFUNGULIWA MASHTAKA YA WIZI

Rapa nyota aliyetamba katika miaka ya nyuma Vanilla Ice amefunguliwa mashtaka yahusuyo wizi huko Lantana, Fla, karibu na mahali anapojenga nyumba kwa ajili ya shoo yake ya uhalisia iitwayo “The Vanilla Ice Project,”.

Ice ambaye jina lake halisi Robert Van Winkle alishikiliwa na polisi jana na kufunguliwa shtaka la wizi uliotokea mwezi uliopita. Mkuu wa kituo cha polisi cha Lantana Sean Scheller amesema katika wizi huo vitu vikubwa vikiwemo hita ya bawa la kuogelea, baiskeli na vitu vingine viliibiwa.

Baada ya kufanya uchunguzi polisi wa Lantana walifanya uchunguzi kwenye nyumba ya jirani ya ile ambayo Vanilla Ice anaifanyia ukarabati na kukuta baadhi ya vitu vilivyoibiwa kwenye nyumba ya Ice na kuvirejesha kwa mwenyewe.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni