Mshambuliaji wa Manchester United
Robin van Persie amemaliza ukame wa magoli baada ya kuifungia timu
yake bao moja na kuisaidia kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya
Leicester City.
Van Persie alifunga bao la kwanza
mnamo dakika ya 27, kabla ya Radamel Falcao kuongeza bao la pili,
ambapo kapteni wa Leicester City Wes Morgan alizidi kulizamisha
jahazi lake kwa kujifunga.
CHELSEA NA MANCHESTER CITY HAKUBA
MBABE
Mechi baina ya Chelsea na Manchester
City imeisha kwa sare ya bao 1-1, matokeo ambayo yanambeba kocha
Jose Mourinho na kikosi chake kuongoza ligi kuu ya Uingereza kwa
tofauti ya pointi tano.
Katika mchezo huo Loic Remy alikuwa
wa kwanza kucheka na wavu, lakini David Silva alisawazisha bao hilo
kabla ya mapumziko na kuisaidia Manchester City kuondoka na pointi
moja katika dimba la Stamford Bridge.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni