Balozi wa Marekani nchini Korea
Kusini, Mark Lippert, amejeruhiwa kwa kisu baada ya kushambuliwa na
mtu mmoja Jijini Seoul.
Bw. Lippert alikuwa amehudhuria
mkutano wa kifungua kinywa wakati alipovamiwa na kukatwa na kisu
usoni na kwenye mkono wake wa kushoto.
Balozi huyo alikimbizwa hospitali
kwa matibabu, na imeelezwa kuwa majeraha yake ni madogo na hayatishii
uhai wake.
Mashahidi wamesema mshambuliaji huyo
mwanaume, ambaye aliwahikuwa mwanajeshi wa taifa la Korea, alipaza
sauti akidai Korea Kaskazini na Korea Kusini ziunganishwe.
Matone ya damu yakiwa yamedondokea kwenye meza aliyokaa balozi huyo
Maafisa usalama wakiwa wamemdhibiti mvamizi huyo
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni