.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 1 Machi 2015

BODI YA MAREFA UINGEREZA YAMKINGIA KIFUA REFA ROGER KWA KUMPA KADI NYEKUNDU YENYE UTATA WEST BROWN

Bodi ya marefa wa kulipwa imesema adhabu ya kutolewa kwa kadi nyekundu beki ya Sunderland Wes Brown katika mchezo wa jana dhidi ya Manchester United si tukio la refa kushindwa kumbaini muhusika.

Refa Roger East alimtoa Brown, kwa kile kinachoonekani ni kwa makosa katika mchezo ambao Manchester United iliibuka nyumbani na ushindi wa mabao 2-0.

Katika tukio hilo picha za televisheni zinaonyesha John O'Shea akimfanyia madhambi mshambuliaji wa Manchester United Radamel Falcao, lakini kadi akapewa Wes Brown.

Hata hivyo Mafisa wa Chama cha Marefa wa Kulipwa Uingereza , wamesema refa East anadhani Brown ndie amemfanyia madhambi Falcao.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni