.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 29 Machi 2015

KIUNGO MAROUANE FELLAINI ATAKATA NA TIMU YA TAIFA YA UBELGIJI

Kiungo wa Manchester United Marouane Fellaini jana usiku aliifungia magoli mawili timu yake ya taifa ya Ubelgiji wakati ikiibuka na ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Cyprus, katika mchezo wa kuwania kucheza michuano ya mabigwa wa bara la Ulaya.

Katika mchezo huo Fellaini alifunga goli la kwanza mnamo dakika ya 21, kabla ya Christian Benteke kupachika la pili dakika ya 35 kufuatia pande kali kutoka kwa kiungo wa Chelsea Eden Hazard.
                                  Benteke akipongezwa na wenzake baada ya kupachika bao.
Wakati huo huo kiungo wa Arsenal, Aaron Ramsey pamoja na winga wa Real Madrid, Gareth Bale waliweza kuiongoza vyema timu ya taifa ya Wales kuwafunga wenyeji Israeli kwa mabao 3-0 katika mchezo mwingine wa kuwania kucheza michuano ya mabigwa wa bara la Ulaya.

Katika mchezo huo uliochezwa kwenye dimba la Ofer mjini Haifa, Bale alimtengenezea bao Ramsey katika kipindi cha kwanza kabla na yeye kucheka na nyavu mara mbili katika kipindi cha pili.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni