Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na baadhi ya Viongozi wa Baraza la Vyuo Vikuu vya Afrika Mashariki, waratibu wa mkutano Mkuu wa Sita wa majadiliano ya kukuza maendeleo endelevu ya mifumo ya Elimu ya Juu na Maendeleo ya Kiuchumi. Mkutano huo ulifunguliwa leo Machi 31, 2015 kwenye Ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifungua rasmi mkutano Mkuu wa Sita wa majadiliano wa Baraza la Vyuo Vikuu vya Afrika Mashariki (IUCEA) wenye lengo la kukuza maendeleo endelevu ya mifumo ya Elimu ya Juu na Maendeleo ya Kiuchumi, uliofanyika leo Machi 31, 2015 kwenye Ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. Baadhi ya washiriki wa Mkutano huo wakimsikiliza makamu wa Rais Dkt. Bilal, wakati akisoma hotuba yake ya ufunguzi wa mkutano huo.
Picha na OMR
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni