.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 27 Machi 2015

MASHIRIKA YA NDEGE SASA KULAZIMISHA MARUBANI KUWA MUDA WOTE KATIKA CHUMBA CHA KURUSHIA NDEGE

Mashirika ya ndege duniani yameanza kutaka marubani wawili kuwapo muda wote katika chumba cha kurushia ndege kufuatia tukio la ajali ya ndege katika Mlima Alps nchini Ufaransa.

Mashirika makubwa ya ndege ya Canada, Norway, Ujerumani pamoja na Uingereza yameahidi kubadili sera zao.

Mamlaka ya Usafiri wa Anga ya Uingereza (CAA) imesema itafuatilia matokeo ya uchunguzi wa ndege Germanairwings, kufuatia kuwepo za taarifa za rubani kuiangusha ndege hiyo makusudi.

Shirika la ndege la Lufthansa limesema hata kama kungekuwa na ulinzi mzuri vipi, hakuna namna ingewezekana kumzuia rubani mwenye nia mbaya.


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni