.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 30 Machi 2015

RAIS WA GUINEA ALPHA CONDE AMETANGAZA SIKU 45 ZA DHARURA ZA KIAFYA

Rais wa Guinea, Alpha Conde ametangaza siku 45 za dharura za kiafya, katika mikoa mitano magharibi na kusini magharibi mwa nchi hiyo kutokana na mlipuko wa Ebola.

Tahadhari hiyo ni pamoja na kuweka karantini kwa hospitali na zahanati ambazo mlipuko mpya wa ugonjwa wa Ebola umebainika, pamoja na taratibu mpya za maziko na kuzuia watu kutoka ndani ya nyumba zao.

Mlipuko wa Ebola ulianza Guinea mwezi Desemba mwaka 2013, ambapo Januari mwaka huu Shirika la Afya Duniani liliripoti kushuka mno kwa matukio ya watu wanaougua Ebola nchini humo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni