Picha ya video imemuonyesha polisi
mmoja nchini Marekani akimpiga risasi na kumuua mtu asiye na makazi
wakati wakibishana nao katika Jiji la Los Angeles.
Picha hizo zinaonyesha mapambano
baina ya mtu huyo na maafisa kadhaa wa polisi katika eneo la Jiji
hilo la Skid Row.
Wakati polisi wakijaribu kumdhibiti,
ilisikika sauti ikimuambia weka silaha chini, na sekunde kadhaa
baadae akapigwa risasi. Polisi bado hawajathibitisha iwapo mtu huyo
alikuwa na silaha.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni