.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 6 Machi 2015

WAGANGA WAPIGA RAMILI CHONGANISHI 32 MBARONI NA ZANA ZA KULAGHAIA GEITA


Jeshi la polisi mkoani Geita linawashilikilia waganga wa kienyeji 32 kwa kupiga ramli chonganishi, ambao wamekutwa na zana zao za kufanyia udangayifu zikiwemo nyara za serikali za wanyama tofauti wakiwemo Kakakuona, Fisimaji, Nyoka waliokaushwa, Sarafu za fedha za aina tofauti, ngozi za chui na mikia ya nyumbu, pembe na kucha za wanyama ambavyo vyote huvitumia kupigia ramli chonganishi.

Aidha, waganga hao wanadaiwa kuendesha upigaji ramli ikiwemo kuwasafisha kwa kuwatoa mikosi wauaji wa walemavu wa ngozi na vikongwe kwa kuwapa dawa za ujasiri na baada ya kutejeleza ukatili huo waganga hao wanadaiwa kuwatengenezea tena dawa wa kuwasafisha kwa kuwatoa mikosi vitendo vinavyodaiwa kuwa chimbuko la mauaji ya kikatili ya kutumia mapanga kwa walemavu wangozi na vikongwe.

Kamanda wa polisi mkoa wa Geita Kamisha msaidzi mwandamizi Joseph Konyo ameyasema hayo leo katika mkutano wake na waandishi wa habari ikiwa ni siku moja tu toka mahakama kuu kanda ya Mwanza kuwahukumu watuhumiwa wanne wa mlemavu wangozi adhabu ya kunyongwa ahadi kufa.

Akitoa uafafanuzi juu ya kutiwa mbaroni kwa watuhumiwa hao Kamanda Konyo amesema waganga hao wamekamatwa katika oporesheni ya siku mbili enedeleu ya juzi na jana ambapo hao ni sehemu ya waganga zaidi ya 2000 wanaoendesha vitendo hivyo vya uchonganishi na utaperi huku wilaya ya Geita peke yake ikikadriwa na kwua nawaganga zaidi ya 900,Wilaya ya Chato waganga 400,Mbogwe waganga zaidi ya 500,Bukombe 600 na Nyang'hwale 300.

Kabla ya baadhi ya waganga kutiwa mbaroni polisi kupitia kitengo cha Upelelezi wa makosa ya jinai na Intelijensia waliweka mitego na kufanikiwa kuwaingiza mtegoni baadhi ya wapiga ramli waonaodai wana uwezo wa kuwawezesha watu kupata utajiri kwa kuchimba dhahabu na bahati ya nyota kwa biashara kwa kuwapigia ramli hatua iliyodaiwa kuwa imekuwa chanzo na uchochezi wa mauaji ya vikongwe na walemavu wangozi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni