.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 5 Aprili 2015

BASI LA TIMU YA FENERBAHCE LASHAMBULIWA KWA RISASI NCHINI UTURUKI

Basi la timu ya Fenerbahce limeshambuliwa na mtu mwenye silaha baada ya mchezo wa Ligi Kuu ya Uturuki ambao walishifunga Rizespo kwa mabao 5-1.

Dereva wa vinara hao wa ligi amekimbizwa hospitali, hata hivyo hakuna hata mchezaji mmoja wa Fenerbahce aliyeumia katika shambulio hilo lililotokea wakati wakielekea katika uwanja wa ndege wa Trabzon.

Waziri Mkuu wa Uturuki Ahmet Davutoglu amesema uchunguzi kuhusiana na tukio hilo unaendelea.

Shirikisho la Soka la Uturuki limelaani shambulio hilo, naye Katibu Mkuu wa timu ya Fenerbahce, Mahmut Uslu amesema tukio hilo ni jambo lisilofaa.
                    Mchezaji wa Fenerbahce akitoa macho asiamini kilichotokea

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni