.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 5 Aprili 2015

ARSENAL YAICHAKAZA LIVERPOOL KWA MABAO 4-1, WAKATI MAN U NA CHELSEA NAZO ZIKISHINDA

Timu ya Arsenal jana imeichakaza Liverpool kwa mabao 4-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Uingereza uliochezwa kwenye dimba la Emirates.

Katika mchezo huo mabao ya Arsenal yalipachikwa kimiani na Hector Bellerin, Mesut Ozil, pamoja na Alexis Sanchez na kuharibu kabisa mahesabu ya Liverpool kuingia katika nafasi ya nne bora.
                                 Kipa wa Liverpool akijaribu kuzuia mpira usiingie langoni
                                       Raheem Sterling ni kama akiashiria kipigo kinatosha 
Nayo Manchester United iliifunga Aston Villa mabao 3-1 katika mchezo uliopigwa katika Dimba la Old Traford, ambapo Wayne Rooney alifunga bao la kiufundi, wakati kiungo Ander Herrera akipachika mawili. Bao pekee la Villa lilifungwa na Christian Benteke.
                                          Wayne Rooney akijipinda kufunga goli lake la ajabu
Na goli la ajabu la Charlie Adam alilolifunga kutoka umbali wa yadi 66 litabakia katika historia ya soko licha ya Chelsea kuifunga Stole mabao 2-1 katika dimba la Stamford Bridge.

Katika mchezo huo Eden Hazard alipachika kimiani bao la kwanza baada ya Cesc Fabregas kuwekwa chini katika eneo la penalti na Loic Remy alikamilisha ushindi wa Chelsea kufuatia makosa ya kipa wa Stoke, Asmir Begovic.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni