.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 9 Aprili 2015

CRISTIANO RONALDO AFIKISHA MAGOLI LA 300 AKIWA NA KLABU YA REAL MADRID

Cristiano Ronaldo amefunga goli la 300 akiwa na klabu ya Real Madrid na kuwa mchezaji wa tatu wa klabu hiyo kufikisha idadi hiyo ya magoli na kuungana na wachezaji Alfredo Di Stefano na Raul.

Mshambuliaji huyo raia wa Ureno alipachika bao dhidi ya Rayo Vallecano katika dakika ya 68 na kuifanya Real kuwa nyuma kwa pointi nne dhidi ya vinara Barcelona, licha ya kupewa kadi kimakosa kwa kujirusha jambo litakalomfanya akose mchezo wa La Liga dhidi ya Eibar.

Mbali na hilo Ronaldo sasa amefikisha mabao 300 katika michezo 288 akiwa na Real na kufanya kile ambacho mshambuliaji anapaswa kufanya, kwa kupiga mpira wa kichwa kwa chini na kumpita golikipa Cristian Alvarez.
                           Ronaldo akianguka chini katika tukio analodaiwa kujirusha 
                                Ronaldo badala ya kupewa penati alilambwa kadi na refa

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni