.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 7 Aprili 2015

KABURI LA PAMOJA LENYE MIILI IPATAO 1,700 LABAINIKA TIKRIT NCHINI IRAK

Kaburi linalohisiwa kuzikwa watu wengi hadi kufikia 1,700 limebainika katika mji wa Tikrit nchini Irak uliotwaliwa kutoka kwa kundi la Dola ya Kiislam (IS).

Eneo hilo lipo karibu na iliyokuwa kambi ya Marekani ya Camp Speicher katika mji wa Tikrit.

Wachunguzi wa matukio ya vifo wa Irak wameanza kufukua na kuhamisha makaburi 12 katika mji huo ambao hivi karibuni umekombolewa kutoka kwa IS.

Mwezi Juni mwaka 2014 kundi la IS linalojulikana kwa vitendo vya ukatili lilituma picha za video kwenye tovuti likionyesha likiwauwa wanajeshi, wengi wakiwa ni waumini wa dhehebu la Shia.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni