Meli ya uvuvi ya Urusi imezama
katika penisula ya Kamchatka, ambapo mabaharia wapatao 54
wamethibitishwa kufa maji hadi sasa.
Watu 63 wameokolewa wengi
wakisumbuliwa na ugonjwa wa baridi yabisi kwa mujibu wa kikosi cha
uokoaji cha wanamaji cha Urusi.
Meli hiyo ya Dalniy Vostok yenye
mfumo wa jokofu ilikuwa na watu 132, wakati ikizama, ambapo miongoni
mwao 78 warusi na wengine waliobakia wakitokea katika nchi za Latvia,
Ukraine, Myanmar pamoja na Vanuatu.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni