.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 3 Aprili 2015

RAIS OBAMA APONGEZA MPANGO WA MAKUBALIANO YA KUZUIA IRAN KURUTUBISHA NYUKLIA

Rais Barack Obama amepongeza mpango wa makubaliano ya kuizuia Iran kuendelea na programu yake ya nyuklia, kuwa ni wa kihistoria, na iwapo utatekelezwa kwa vitendo utaifanya dunia kuwa salama.

Mpango wa utekelezaji wa makubaliano hayo umefikiwa baada ya mazungumzo ya kina, yenye lengo la kuizuia Iran kutengeneza silaha za nyuklia ili iondolewe vikwazo ilivyowekewa.

Irani na mataifa sita yenye nguvu duniani yaliyohusika katika mazungumzo hayo sasa yanangojea hatua ya kukamilisha mpango huo.

Raia wa Iran wamekuwa wakisherehekea mitaani mpango huo, lakini kwa upande wake Israeli imesema makubaliano hayo yanatishia uwepo wa Israeli.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni