Bondia Floyd Mayweather ( kushoto ) akijifua na Uncle Roger kabla ya pamabano lake.
Bondia Manny Pacquiao ( kulia ) akijifua chini ya mkufunzi wake Freddie Roach kabla ya pambano lake.
Hatimaye tiketi kwa ajili ya mashabiki watakaotaka kwenda kushuhudia pambano linalosubiriwa kwa hamu kubwa kote ulimwenguni kati ya mabondia Floyd Mayweather na Manny Pacquiao zimeanza kuuzwa toka jana jumatano.
Zaidi ya tiketi 1000 zitauzwa kwa kati ya dola za kimarekani 1,500 hadi dola 7,500 kwa tiketi moja.
Ukumbi wa MGM Grand Arena ambako pambano hilo ndipo litakapofanyika May 02'2015 unauwezo wa kuchukua watazamaji 16,500.
Hata hivyo nyingi ya tiketi hizo zinatarajiwa kuuzwa kwa kambi mbili tofauti zinazowaunga mkono mabondia hawa.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni
(
Atom
)


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni