.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 2 Aprili 2015

TIMU YA TAIFA YA NGUMI YATAJWA


Hatimaye baada ya mchakato wa muda mrefu, uliofanyika kwa umakini kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa hatimaye Shirikisho la Ngumi Tanzania (BFT) limepata wachezaji wa timu ya Taifa ya Ngumi 2015. 

Katika mashindano ya kimataifa yaliyoshirikisha timu za taifa kutoka Uganda na Kenya, mashindano yaliyomalizika kwa mafanikio, Jumamosi ya tarehe 28.03.2015 uwanja wa Taifa wa ndani .

Mabondia waliochaguliwa kwa sasa taratibu za kuombewa ruhusa katika timu zao zinafanyika na taratibu hizo zitakapo kamilika watatakiwa kuanza mazoezi kabla ya tarehe 15.04.2015, kwa ajili ya kushiliki mashindano mbalimbali ya kitaifa na kimataifa hasa mashindano ya Michezo ya Afrika (All African Games) Septemba 4-19. Brazzaville Congo. 


Na mashindano ya Ubingwa wa Dunia (AIBA World Boxing Championships) Octoba 5-18 Doha Qatar.

Mabondia waliochaguliwa kwa uzito wao ni kama ifuatavyo:-
                                                                             
                                                                                    49 kgs L/FLY

· Mohamed Mzeru –JKT

· Maulid Athumani-

· Ibrahim Abdalah – Magereza.

                                                                               52 Kgs Fly Weight.

· Juma Ramadhani- Temeke

· Said Hofu- JKT

                                                                        56 Kgs Bantam Weight

· Ahamad Furahisha- JKT

· Bon Mlingwa- JKT

                                                                            60 Kgs Light weight.

· Elias Mkomwa- JKT

· Bosco Bakari- JKT

· Fabian Gaudence- NGOME

                                                                           64 Kgs Light Weight
· Kassim Mbwitike- JKT

                                                                         69 Kgs. Welter Weight.

· Said Gulushad – JKT

· Seleman Bamtulah- JKT

                                                                         75 Kgs Middle Weight.

· Ivan Mussa – Kagera

                                                                             81 Kgs light Heavy

· Hamidu Halfan-JKT

                                                                           91 Kgs Heavy weight

· Alex Sitta- JKT

· Nuru Ibrahim- Magereza

Aidha BFT inawapongeza Mabondia wote kwa jitihada kubwa walizofanya na hatimae kuchaguliwa kuwa mabondia wa timu ya taifa ya ngumi 2015.
                                                          
                                                             Nakala kwenu kwa Taarifa. 
                                                                      Makore Mashaga 
                                                                   Katibu Mkuu (BFT)

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni