Mamia ya waombolezaji wamejitokeza na kuwasha mishumaa sehemu mbalimbali nchini Italia kama ishara ya kuwakumbuka zaidi ya wahamiaji 900 waliofariki dunia katika pwani ya Libya wakiwa wanajaribu kuvuka bahari ya Mediterranean kwenda Ulaya kutafuta maisha bora.
Wahamiaji hao walipoteza maisha yao baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuzama. Taarifa zinasema mpaka sasa zaidi ya wahamiaji 1,800 wamefariki dunia katika bahari ya Mediterranean mwaka huu pekee walipokuwa wakijaribu kwenda Ulaya kwa kutumia boti.
Mmoja wa waombolezaji akilia kwa uchungu wakati wa kuwasha mishumaa ya kuwakumbuka wahamiaji waliofariki dunia baada ya boti yao kuzama baharini wiki iliyopita.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni