.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 13 Mei 2015

MAJENERALI WA JESHI LA BURUNDI WAMEMPINDUA RAIS PIERRE NKURUZINZA

Majenerali wa Jeshi la Burundi wamempindua rais Pierre Nkuruzinza, huku taifa hilo likiendelea kuwa na machafuko kutokana na uamuzi wake wa kutaka kuwania urais kwa muhula wa tatu.

Meja Jenerali Godefroid Niyombareh amesema kamati ya taifa ya kulikomboa taifa hilo imeundwa ili kuiongoza nchi hiyo.

Hata hivyo haijafahamika mara moja iwapo Meja Jenerali Niyombraeh anaungwa mkono kwa kiasi gani na maafisa wengine wa jeshi.

Rais Nkuruzinza ambaye yupo nchini Tanzania ingawa hajaonekana katika mkutano wa wakuu wa nchi za Afrika Mashariki unaojadili mgogoro wa nchi yake. Msaidizi wake ameelezea mapinduzi hayo kuwa ni mzaha.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni