.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumamosi, 23 Mei 2015

MWANAMKE WA MIAKA 65 AJIFUNGUA WATOTO WATATU NCHINI UJERUMANI

Mwanamke mwenye umri wa miaka 65 nchini Ujerumani amejifungua watoto watatu baada ya kutunga mimba kwa njia za kupandikiza kisayansi.

Kituo cha runinga cha RTL nchini Ujerumani kimesema mwanamke huyo Annegret Raunigk, amejifungua watoto wawili wa kiume na mmoja wa kike kwa njia ya upasuaji Jijini Berlin.

Watoto hao wamezaliwa kabla ya muda wao wakiwa na wiki 26, hata hivyo madaktari wamesema wote wapo katika hali nzuri ya kuweza kuishi.

Annegret Raunigk ambaye alikuwa na watoto 13 pamoja na wajukuu saba, ameweka rekodi ya kuwa mwanamke wa kwanza duniani mwenye umri mkubwa kujifungua mapacha watatu.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni