Mabondia Manny Pacquiao na mpinzani wake Floyd Mayweather jana wamepima uzito kabla ya pambano lao linalosubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa mchezo huo kote ulimwenguni, pambano ambalo litapigwa kesho alfajiri.
Pambano hilo litafanyika katika ukumbi wa MGM Grande Garden Arena mjini Las Vegas nchini Marekani. Mabondia wote kila mmoja ametamba kuibuka na ushindi dhidi ya mwenzake.
Mayweather raia wa Marekani ana umri wa miaka 38, ana urefu wa futi 5.8 na katika rekodi ya mapambano yake, ameshinda yote 47, hajawahi kupigwa.
Kwa upande wa Manny Pacquiao maarufu kama Pacman raia wa Ufilipino, ana umri wa miaka 36, ana urefu wa futi 5.6.
Katika mapambano aliyopigana, ameshinda mara 57, amepigwa mara 5 na sare mara 2.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni