.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 14 Mei 2015

SASA NI WAZI FAINALI LIGI YA MABINGWA BARANI ULAYA NI FC BARCELONA NA JUVENTUS, REAL MADRID YAVULIWA UBINGWA MBELE YA MAELFU YA MASHABIKI WAKE SANTIAGO BERNABEU

Mabingwa watetezi wa kombe la ligi ya mabingwa barani Ulaya, timu ya soka ya Real Madrid ya Hispania usiku wa kuamkia leo wamevuliwa ubingwa huo na bibi kizee cha Turin, Juventus ya Italia baada ya kulazimishwa sare ya kufungana bao 1-1. 

Katika mchezo huo wa marudiano wa hatua ya nusu fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya, Juventus imesonga mbele kwa idadi ya mabao 3-2. Katika mchezo wa kwanza uliochezwa Italia, Juventus iliifunga Real Madrid magoli 2-1.
Katika mchezo wa usiku wa kuamkia leo, Madrid wakicheza mbele ya maelfu ya mashabiki wao walijitahidi kulisakama lango la wapinzani wao lakini uimara wa kipa mkongwe wa Juventus, Buffon uliwanyima nafasi nyingi za kufunga goli. 

Bao lao lilipatikana kwa mkwaju wa penati uliofungwa na Cristiano Ronaldo katika dakika ya 23, bao lililodumu hadi kipindi cha kwanza kinamalizika. 

Kipindi cha pili Juventus walikuja juu na kusawazisha bao hilo kupitia kwa Alvaro Morata kunako dakika ya 57.
Kwa matokeo hayo, Real Madrid waliokuwa mabingwa watetezi wa kombe hilo wamevuliwa ubingwa huo, na sasa fainali itazikutanisha FC Barcelona ya Hispania na Juventus ya Italia. Mchezo wa fainali utachezwa June 06' 2015 mjini Berlin, nchini Ujerumani.
TUNAWASHUKU SANA, TUKUTANE BERLIN!! Wachezaji wa Juventus wakiwashukuru mashabiki wao baada ya kumalizika kwa mchezo wao dhidi ya Real Madrid.



Hakuna maoni :

Chapisha Maoni