.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 22 Mei 2015

VIKOSI VYA ULINZI KENYA VYA TIBUA JARIBIO LA SHAMBULIO LA KIGAIDI LA AL-SHABAAB


Vikosi vya ulinzi Kenya jana jioni vimetibua jaribio la shambulio la kigaidi lililopangwa na wapiganaji wa kundi la Al-Shabaab kwenye kijiji cha Yumbis katika kaunti ya Garissa.

Waziri wa Mambo ya Ndani imesema wanakijiji walitoataarifa kwa vikosi vya usalama, kuwa wameona wapiganaji wenye siala majira ya saa 12 jioni.

Msemaji wa Wizara hiyo Mwenda Njoka ameleza kuwa vikosi vya usalama viliwavamia wapiganaji hao na kupambana nao, hata hivyo hakukuwa na taarifa za kuwepo mtu aliyejeruhiwa.

Mkuu wa Jeshi la Polisi Kenya Joseph Boinnet, amesema wapiganaji wa Al-Shabaab, wanawaghasi wananchi, lakini vikosi vya usalama vimewatimua.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni