.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 13 Mei 2015

VILABU 15 VYA SOKA KENYA VYA LIGI KUU VYAPIGWA FAINI

Klabu 15 za Ligi Kuu ya Kenya (KPL) zimepigwa faini na wasimamizi wa ligi kuu ya nchi hiyo zinazofikia kiasi cha shilingi 1, 560, 000 ambazo zinapaswa kulipwa hadi Ijumaa ya tarehe 15 mwezi huu.

Mabigwa wa Ligi hiyo klabu ya Gor Mahia na wapinzani wao wa jadi timu ya Leopards wameagizwa kulipa kiasi cha shilingi za 240,000 na 200, 000 kutokana na kufanya makosa mbalimbali.

Klabu zingine zilizopigwa faini ni pamoja na Ingwe na K’Ogalo zilizopigwa faini ya shilingi 60, 000 na 50, 000 kwa kushindwa kuwasilisha orodha ya wachezaji wake kwa kampuni yenye haki ya kutangaza ligi kuu ya Kenya.

Gor Mahia pia imepigwa faini ya shilingi 100, 000 ya Kenya kwa kocha wao Frank Nuttal, kushindwa kufanya mahojiano na watangazaji wakuu wa ligi hiyo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni