.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 13 Mei 2015

WATU WAPATAO 43, WAMEUWAWA PAKISTANI KATIKA SHAMBULIO LA KUTUMIA SILAHA

Watu wapatao 43, wameuwawa na wengine 20 kujeruhiwa katika shambulio la kutumia silaha kwa watu waliokuwa katika basi wa dhehebu la Kiislam la Shia Mjini Karachi, nchini Pakistan.

Polisi nchini Pakistan wamesema washambuliaji hao wa kundi lenye itikadi kali lililopigwa marufuku waliokuwa kwenye pikipiki walilisimamisha basi hilo na kuanza kuwafyatulia risasi abiria.

Watu wenye silaha wapatao sita walilishambulia basi hilo lililokuwa na abiria 60, likielekea katika eneo la ibada la Ismaili Shia kwa ajili ya kufanya ibada.

Waumini wa Kiislam wa dhehebu la Shia ambao ni kidogo nchini Pakistan wamekuwa wakihsmbuliwa mara kwa mara na wapiganaji waumini wa dhehebu la Sunni.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni