Wahamiaji kutoka Myanmar wamekwama
wakiwa kwenye boti kwa wiki moja katika bahari ya Andaman wakiwa
hawana chakula ama maji ambapo wenzao kumi wamekufa huku wengine
wakiishi kwa kunywa haja ndogo.
Boti hiyo ya uvuvi iliyokuwa na
wahamiaji hao 350 wa jamii ndogo ya waislamu wa Rohingya,
wamekataliwa kuingia nchini Thailand. Miili ya watu waliokufa ilibidi
waitupe majini.
Wahamiaji hao wameviambia vyombo vya
habari kuwa waliokuwa wanaongoza boti hiyo wamewatelekeza na kuharibu
injini.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni