.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 14 Mei 2015

BARAZA LA USALAMA LA UMOJA WA MATAIFA KUFANYA MKUTANO WA DHARURA LEO

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo litafanya mkutano wa dharura wa majadiliano kuhusu Burundi, baada ya jenerali mwandamizi kutangaza kuwa rais Pierre Nkurunziza ameondolewa madarakani.

Ufaransa imeitisha mkutano huo ambao utafanyika mara tu baada ya kikao cha mazungumzi yanayohusu Irak, rais wa baraza hilo wa kutokea Lithuania ameeleza.

Taifa la Burundi limetumbukia zaidi katika taharuki baada ya Jenerali Godefroid Niyombare, ambaye aliwahi kuwa mkuu wa usalama wa taifa hilo mwenye nguvu kutangaza kung'olewa rais Nkuruzinza, wakati rais akiwa nchini Tanzania.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni