.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 14 Mei 2015

WATU 72 WAFA KWA MOTO KATIKA KIWANDA CHA VIATU NCHINI PHILIPPINE

Idadi ya vifo vilivyotokana na moto ulioteketeza kiwanda cha viatu nchini Philippine imefikia watu 72.

Polisi nchini humo wameahidi kuwachukulia hatua wale wote waliohusika na tukio hilo, huku wafanyakazi wakidai uwepo wa mazingira duni ya afya pamoja na kutofuatwa kwa viwango vya usalama.

Kaimu Mkuu wa Jeshi la Polisi la Philippine, Leonardo Espina amesema chanzo cha moto huo ni cheche ya moto iliyoruka kutoka katika mashine ya kuchomelea na kutumbukia kwenye kemikali zenye kulipuka karibu mlango wa kuingilia kiwandani.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni