.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 14 Mei 2015

RUTO AMTAKA RAILA ODINGA KUTOMUHUSISHA NA MATUKIO YA RUSHWA

Naibu rais wa Kenya Bw. William Ruto amemtaka kiongozi wa chama cha CORD, Raila Odinga kuacha kuhusisha jina lake na kashfa za rushwa, na kumuonya kuwa yupo tayari kuanzisha vita ya kisiasa na yeye.

Bw. Ruto amemtuhumu Odinga pamoja na aliyekuwa msaidizi wake, Bw. Herbet Ojwang kwa kumuhisisha na rushwa ya mradi wa shilingi bilioni 17 za Kenya, wa kuikarabati Hospitali ya Rufaa ya Chuo cha Mafunzo Moi iliyopo Eldoret.

Mradi huo unachunguzwa na Kamati Uwekezaji ya Umma (PIC) kutokana na tuhuma kuwa gharama ziliongezwa na kwamba Ruto alitumia ushawishi wake kumtoa Bw. Ojwang katika mradi huo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni