Mkurugenzi wa taasisi ya Taifa ya
utafiti wa magonjwa ya binadamu Dkt. Mwelechele Ntuli Malecela
amechukua fomu kwa ajili ya kuomba ridhaa ya kupeperusha bendera ya
chama hicho kwenye nafasi ya urais.
Dkt. Malecela ambaye ni mtoto wa
Waziri Mkuu wa zamani John Malecela amekuwa mwanamke wa pili kuchukua
fomu ya kuwania urais kupitia CCM baada ya Balozi Amina Salum Ally
kuchukua fomu wiki iliyopita.
Dkt Malecela amesema kuwa kama
atapewa ridhaa ya kuwania nafasi ya urais kupitia CCM atawawezesha
wanawake nchini kushika nafasi mbalimbali za uongozi katika ngazi za
maamuzi kwani awamu hii ya nne imewapa upendeleo wa kutosha.
Amesema kwa sasa hawezi kuahidi kuwa
atawafanyia nini Watanzania hadi pale atakapopewa ridhaa na chama
chake ambapo atatekeleza vipaumbele vilivyoko katika ilani ya chama
chake, hata hivyo amesema atahakikisha kuwa huduma za afya, elimu ya
ufundi, uchumi na kuudumisha muungano ambayo ni tunu ya Taifa
vinatekeleza kwa uhakika.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni