Polisi nchini Marekani wanawahoji
wafanyakazi katika gereza moja lenye ulinzi mkali Jijini New York
kufuatia tukio la kutoroka kwa wafungwa wawili wa mauaji.
Gavana wa Jiji hilo Andrew Cuomo
amesema mamia ya wafanyakazi na wajenzi wa gereza hilo wanachunguzwa
kubaini iwapo waliwasaidia wafungwa hao vifaa walivyotumia kutorokea.
Wafungwa Richard Matt, 48,na David
Sweat, 34, walitumia vifaa vyenye uwezo mkubwa kuvunja gereza la
Clinton lililopo Dannemora siku ya Ijumaa.
Bomba walilotoboa wafungwa na kupita ndani kutokea nje ya gereza
Hapa ndipo walipoibukia na kutokomea mitini



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni