.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 15 Juni 2015

IDARA YA SHERIA YA AFRIKA KUSINI YAJIPANGA KUMDHIBITI RAIS AL BASHIR

Idara ya sheria ya Afrika Kusini inajiandaa kwa ajili ya malumbano ya kisheria katika Mahakama Kuu ya Pretoria, huku kukiwepo kwa taarifa kuwa rais Omar al-Bashir wa Sudan ameondoka Afrika Kusini jana usiku.

Licha ya taarifa za kuondoka kutothibitishwa, suala la kuondoka Afrika Kusini litakuwa ni kinyume na amri ya Mahakma Kuu ya Pretoria ambayo jana mchana iliishinikiza mamlaka ya Afrika Kusini kutomruhusu rais al-Bashir kutoondoka nchini.

Msemaji wa Idara ya sheria Wakili Mthunzi Mhaga, amesema hakuna uthibitisho kuwa rais Al-Bashir ameondoka nchini humo.

Wakati al-Bashir akiendelea kuhudhuria vikao cha Umoja wa Mataifa kwa uhuru si mbali sana kutoka Mahakama Kuu ya Pretoria, vyombo vya haki za binadamu vimekuwa vikipambana kuhakikisha anakamatwa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni