.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 14 Juni 2015

MAFURIKO YASABABISHA WANYAMA KUTOROKA KWENYE ZOO

Mafuriko makubwa yamelikumba Jiji Kuu la Tbilisi nchini Georgia na kuuwa watu wanane, ambapo maafisa wa nchi hiyo wamewaonya wananchi kutotoka nje ili kuepuka kukutana na wanyamapori waliotoroka kwenye eneo la kufugia wanyamapori.

Wanyama hao ambao hawajulikani walipo ni duma, simba, dubu pamoja na mbweha, ambapo pia inasadikiwa kwamba muangalizi wa wanyama hao amekufa.

Kiboko mmmoja amefanikiwa kudhibitiwa katika eneo kuu la mapumziko la Jiji Tbilisi na kupigwa na bunduki yenye sindano ya usiongizi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni