Makumi ya watu wamekamatwa nchini
Morocco kwa kutenda kosa la kuuza majibu ya mtihani wa taifa wa
kidato cha sita katika hali ambayo pia imepelekea majibu ya mitihani
miwili kuwekwa kwenye ukurasa wa Facebook.
Mkurugenzi Mkuu wa Usalama wa Taifa
amesema watu 57 wamekamatwa katika miji 15 wakiuza majibu ya mtihani
ambapo kwa baadhi ya mitihani majibu yalikuwa yakitumwa kwa wanafunzi
kwa kutumia ujumbe mfupi wa maandishi.
Mkurugenzi Mkuu huyo amesema kwamba
watu waliokamatwa wanatuhumiwa kutoa majibu yaliyoandikwa tayari kwa
wanafunzi na kujipatia fedha.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni