Bondia Mmarekani Deontay Wilder
ametetea taji lake la uzito wa juu duniani la WBC baada ya kufanikiwa
kumtwanga kwa knockout bondia Eric Molina katika raundi ya tisa.
Bondi huyo mwenye umri wa miaka 29,
ambaye alimpiga Bermane Stiverne mwezi Januari na kuwa Mmarekani wa
kwanza kutwaa taji la uzito huo tangu mwaka 2007, hajapigwa katika
mapambano 34 aliyocheza.
Molina, mwenye umri wa miaka 33,
ambaye amepoteza michezo yake miwili kati ya 25, aliangushwa chini
katika raundi ya nne, na mara mbili tena katika raundi ya tano,
ambapo alisalimu amri katika raundi ya tisa ndipo na kushindwa
kuendelea na pambano.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni