Mahakama kaskazini mwa Nigeria
imemuondolea mashtaka msichana wa miaka 14 anayetuhumiwa kutumia sumu
ya panya kumuua mumewe mwenye umri wa miaka 35.
Serikali ya jimbo la Kano, imeomba
kesi hiyo kufutwa kutokana binti huyo ni mtoto ambaye alilazimishwa
kuolewa katika umri mdogo.
Mtoto huyo wa kike sasa ataachiwa
huru kufuatia uamuzi huo wa mahakama.
Kesi yake iliporipotiwa mwaka 2014
iliibua angalizo juu ya tatizo la watoto wanaolazimishwa kuolewa
nchini Nigeria.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni