Afisa wa polisi nchini Marekani
ambaye alipigwa picha ya video akimpiga mweleka msichana mweusi na
kumuangusha aridhini na kisha kumuelekezea bastola Jijini Texas
amejiuzulu kazi.
Taarifa zinaeleza afisa huyo Eric
Casebolt, amewasilisha barua ya kuacha kazi bila ya kushinikizwa na
mtu hapo jana.
Katika video hiyo iliyorekodiwa
Ijumaa huko McKinney polisi Casebolt, ambaye ni mzungu alionekana
akimkandamiza chini kwa kutumia magoti binti mweusi wa miaka 15
aitwae Dajerria Becton.
Polisi wamesema afisa huyo alikuwa
ameenda kutuliza ghasia katika sherehe iliyokuwa ikifanywa kwenye
bwawa la kuogelea katika eneo hilo.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni