Mahakama ya nchini Misri imeunga
mkono adhabu ya kifo iliyotolewa kwa rais aliyeng'olewa madarakani wa
nchi hiyo Mohammed Morsi, kwa kosa la kusababisha kutoroka kwa
wafungwa wengi.
Hukumu hiyo ilitolewa awali mwezi
Mei, sasa imethibitishwa baada ya majadiliano na viongozi wa kidini
wa juu wa Misri pamoja na Mufti Mkuu.
Hukumu ya kifo kwa viongozi wakuu wa
chama cha Muslim Brotherhood, akiwemo kiongozi wao mkuu Mohammed
Badie, pia nayo imeridhiwa kutekelezwa.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni