Korea Kaskazini imesema inakabiliwa
na ukame mbaya kuwahi kutokea katika karne, na kuibua hofu ya uhaba
mkubwa wa chakula katika taifa hilo.
Shirika la Habari la Taifa la nchi
hiyo (KCNA) limesema mikoa inayoongoza kwa kilimo cha mpunga
imeathiriwa vibaya na ukame huo.
Mamia kwa maelfu ya raia wa Korea
Kaskazini wanaaminika kufa wakati wa ukame mkubwa uliotokea katika
mwaka wa 1990.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni