Idara ya hazina ya Marekani, imesema
noti ya dola 10 inayobuniwa kwa mara ya kwanza itakuwa na sura ya
mwanamke, lakini haijaamuliwa mwanamke huyo atakuwa nani.
Noti hiyo mpya ya dola kumi
itatolewa mwaka 2020 katika kuadhimisha miaka miaka 100 ya mabadiliko
ya 19 ya Katiba, ambayo yalimpatia mwanamke haki ya kupiga kura.
Hazina ya Marekani itahitaji
michango ya wananchi katika uchaguzi wa mwanamke huyo ambaye
anamchango mkubwa katika demokrasia ya kuhusisha makundi yote.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni