.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 18 Juni 2015

IDADI YA WATU WALIOKIMBIA VITA NA MACHAFUKO YAONGEZEKA DUNIANI

Ripoti ya Umoja wa Mataifa imesema idadi ya watu wasiokuwa na makazi kutokana na vita, migogoro ama mauaji ya visasi imefikia rekodi ya juu ya watu milioni 60 duniani kote.

Taarifa ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuwahudumia Wakimbizi Duniani, UNHCR, imesema idadi ya watu waliolazimishwa kukimbia nyumba zao imeongezeka kwa watu milioni 8.3 kutoka mwaka jana.

Machafuko ya nchini Syria inaonekana kama chanzo kikuu cha ongezeko la idadi ya watu wasio na makazi duniani. Mkuu wa shirika la UNHRC Antonio Guterres amesema dunia imechafuko.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni