Watu tisa wameuwawa katika tukio la
kutumia risasi kwenye kanisa la kihistoria la Wamarekani wenye asili
ya Afrika huko Charleston katika jimbo Marekani la South Carolina.
Mkuu wa polisi wa mji huo Gregory
Mullen amesema watu hao nane wameuwawa wakiwa ndani ya kanisa la
Emanuel African Methodist Episcopal jumatano jioni, ambapo mtu mmoja
mwingine alifariki
Mauaji hayo yameelezwa kuwa
yanatokana na chuki za kibaguzi na polisi wametoa picha za muhusika
kijana mweupe zilizorekodiwa na kamera za usalama.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni