.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 11 Juni 2015

MBUNGE WA MVOMERO, MH AMOS MAKALLA AKABIDHI PIKIPIKI TANO KWA AJILI YA KATA TANO JIMBONI MWAKE

Mbunge wa Mvomero, Mh Amos Makalla akihutubia wajumbe wa halmashauri kuu ya wilaya. 

Mbunge wa Mvomero Mh Amos Makalla amekabidhi pikipiki tano kwa kata mpya tano za Chama cha mapinduzi ili kuwasaidia watendaji na viongozi wa Chama kufanya kazi za Chama kwa wepesi na ufanisi.
 
Akimkambidhi pikipiki hizo, Mbunge wa Mvomero alimueleza mwenyekiti wa wilaya ya Mvomero ndugu Abdalah Mtiga, kuwa msaada huo ni muendelezo wa kukisaidia Chama wilaya ya Mvomero kwani awali alisaidia pikipiki 23, na hizo 5 inafanya jumla ya pikipiki alizosaidia Chama ni 28 zenye thamani ya sh 56,000,000.
 
Akipokea msaada huo, mwenyekiti wa wilaya ndugu Abdalah Mtiga alimshukuru sana mbunge huyo kwa Moyo wake wa kukipenda Chama, kwani ni wabunge wachache sana wenye Moyo kama wa mbunge Amos Makalla. 

Aliwataka watendaji kutunza pikipiki hizo na zitumike kwa shughuli za chama na si vinginevyo


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni