.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 10 Juni 2015

MH MAKALLA APONGEZWA KWA KUFANIKISHA UJENZI WA UKUMBI WA MIKUTANO WA CHUO CHA UALIMU MHONDA

Pongezi hizo alizitoa jana mbele ya  wajumbe wa halmashauri kuu ya kata ya Mhonda  waliokuwa na kikao na mbunge wao. 

Katika maelezo yake, mkuu wa chuo aliwakaribisha ukumbini hapo kwa kumpongeza mbunge kwa mchango mkubwa ambapo alisema,

" viongozi wa kata jana mliniomba kukodi ukumbi tukawaruhusu, ila kwakuwa mbunge yupo hapa naomba niseme na hata viongozi wa wizara ya Elimu niliwaambia kuwa mdau mkubwa aliyechangia vifaa ikiwemo nondo, saruji na mabati zaidi ya asilimia 70 ya ujenzi ni Mhe Makalla, tunakushukuru na kama utakavyoona jina la ukumbi tumeandika hapa inaitwa Makalla Hall, hakika tunakushukuru sana" alisema.
 
Akiwahutubia wajumbe wa halmashauri kuu ya kata ya Mhonda, Mh Makalla aliwaambia kuwa anamshukuru mkuu wa chuo kwa pongezi, na wajumbe wameona kwa macho ukumbi ulivyo mzuri na kwa kuboresha mazingira hayo sasa hata chuo kimepata hadhi kutoka kutoa cheti sasa wameruhusiwa wameanza kupokea wanafunzi wa diploma.
 
Amewaeleza amefanya mambo mengi ya maendeleo katika sekta ya Elimu ikiwemo kuchangia ujenzi wa sekondari zote jimbo la Mvomero, amesaidia vitabu vya sayansi katika sekondari zote wilaya ya Mvomero, amechangia sh 21,000,000 ujenzi wa Maabara kwa sekondari 21 kila sekondari shilingi milioni moja, na pia amewasaidia kompyuta na printa Saccos ya walimu wilaya ya Mvomero.
 
Katika tukio la aina yake, mbunge huyo alijumuika na wanachuo kupata chakula cha pamoja kitendo kilichowafurahisha viongozi wa Chuo, Chama na wanachuo.


Hakuna maoni :

Chapisha Maoni